Language:

Sheriya ya Amerika: Uongozi wa Sheriya

Amerika inaongozewa na système yenyi kutaka usawa wa inchi na ba raiya balindwe na sheriya na banachukuwa mipango fulani ili hizo sheriya ziheshimiwe. Hiyo watu wanaiita “uongozi wa sheriya”. Sheriya mu Amerika zinafata kanuni na haki zenyi kuandikwa ndani ya katiba (constitution) ya Amerika. Watu wote hapa Amerika, pamoja na wakimbizi banalindwa na sheriya hizo na biko na mzigo wa kuzijuwa na kuziheshimu. Jifunze Zaidi hapo chini.

Rights and Responsibilities in the United States

Chagua muundo wa jinsi ambavyo ungependa kupata kwenye ukurasa huu. Unaweza kutazama video, kupakua hati ya maelezo au kusikiliza podikasti. Kila chaguo linatoa maelezo sawa.

Uongozi Wa Batu, Uongozi Unatembezwa Na Batu, Uongozi Ju Ya Batu

Hiyo maneno yenyi kuonesha namuna ya ajabu demokrasia ni kusema nini kabisa, ilisemewa na Raisi Abraham Lincoln mu mwaka wa 1863 wakati vita yenyi ba raiya ba Amerika balikuwa bakipigana kwa benyewe kwa benyewe ilianza fika mwisho. Mu demokrasia, serkali inaongozwa na bashimamizi benyi balichaguliwa na banashimamiya batu benyi balibachagula. Kupitiya habo bashimamizi benyi balichaguliwa, na kupitiya njiya ya uchaguzi na matendo zingine za urahiya, ba raiya banapewa uwezo wa kutengeneza sheriya zenyi zitabaongoza na zitabalinda. Kushurulikya kama raiya byenyi kupita mu inchi ni haki ya lazima saana n ani mzigo w aba raiya bote.

Sheriya Zinatengenezwa Namna Gani?

“Amerika ni ma inchi mingi jimejitaya pamoja; hizo inchi ndogo 50 za Amerika zina kila inchi serkali yake, na kila muji ndani ya kila inchi iko na uongozi wake wa pekee. Sheriya za inchi mzima zinawekwa mbele na zina pangwa na chumba cha serkali ya Amerika chenyi kushurulikiya sheriya (Congress), na zinashikwa na chumba cha uongozi (Raisi na departements za serkali na shirika zingine za serkali), na hizo sheriya zinatumikishwa na chumba cha kutawalisha haki (sistemu ya mahakama ya inchi mzima, moya ya kati ni mahakama kuu [Court Supreme]). Katiba (Constitution) inaamuwa kujuwa kama kipande fulani ya sheriya ni mzigo wa serkali ya inchi yote, ao serkali inchi ndogo fulani ao kama ni mzigo wa serkali ya muji (administration locale).

Kupitiya hiyo hiyo sistemu ya kutengeneza sheriya, chumba ya uongozi wa inchi, na chumba yakutumikisha sheriya, serkali za inchi ndogo zinatumika kwa kuwa na mwangaza kuhusu sheriya fulani na kuheshimisha hizo sheriya zenye zimetengenezwa na serkali ya inchi nzima (gouverment fédéral), na zinaongeza sheriya zingine za kuongoza inchi zabo zidogo. Inchi zidogo zinashimika serkani za muji na zinawapa uwezo ya kufanya piya sheriya zingine. Na kwasababu serkali ya inchi nzima, serkali za inchi ndogo na serkali za miji zinatengenezaka sheriya, inafika sheriya kuwa tafauti wakati uko mu inchi ndogo fulani ao fulani, piya sheriya zinaweza kuwa tafauti ukiwa mu muji fulani ao fulani. Hiyi ni lazima wakimbizi baisikiye kwa sababu mutu wowote anaazimishwa kuheshimu serkali ya inchi ndogo na za muji kwenyi banaishi.

Nani Ataongozwa Na Sheriya?

Hakuna mutu mwenyi haongozwe na sheriya Amerika hata akuwe mheshimiwa saana, ao akuwe na makuta mingi, ao hata akuwe na bukubwa ingine. Sheriya ni zimoya kwa batu bote. Kupana bituliro kwa kuzunguruka sheriya ni kuvunja sheriya na hata kupima kupatiya mtumishi wa serkali kituliro kusudi akufanyiye kitu fulani inayokatazwa ao afunge mecho ku makosa fulani umefanya ni makossa yenyi utapatiliwa malipizi.

Mara mingi Kusitojuwa sheriya haifunikiye mutu. Batu benyi kuvunja sheriya bila kujuwa banapashwa azibiwa, hata kama habakukuwa na niya yakuvunja sheriya.

Haki Yakusambishwa Kama Ginsi Sheriya Inaomba

Ikiwa mutu amevunja sheriya, huyo mutu iko na haki yakusambishwa kwa kweli kama ginsi sheriya inaomba. Haki yakusambishwa kama ginsi sheriya inaomba ni haki ya yakusambisha kwa usawa bakifatililiya procédure fulani ikiwa mutu alifanya kosa. Hapa Amerika, haki ya kusambishwa kwa kweli kama ginsi sheriya inaomba iko ndani ya sura ya tano ya katiba ya Amerika, na banaongeza ingine hakikisho ya kusambishwa kwa kweli ndani ya sura ya sita na sura ya kumi na ine.

Rights and Responsibilities in the United States
Rights and Responsibilities in the United States

Sura ya tano

Sura ya tano inashimika haki ya kusambishwa kama vile sheriya inaomba ikiwa mutu alichongelewa kama alifanya kosa ao kama faida za kitu cha mutu zinataka kubebwa na serkali. Inakataza mutu ashikwe mara pili ju ya kosa moya alifanya. Piya, inasema kama mutu hawezi kuwa shahidi (temoin) mu kesi yake ndani ya mahakama, na kama kitu ya mutu haiwezi chukuliwa kutumikishwa kama kitu ya serkali bila huyo mutu alipiwe kwa haki.

Sura ya sita

Sura ya sita inasema kama mutu aliye chongewa kufanya kosa fulani ana haki ya kusambishwa haraka na wazi, na asikilizwa na juri yenyi haimuoneleye, na awe na mtetezi (Avocat). Piya mutu, mwnaume ao mwanamuke ana haki ya kujulishwa nini banamuchongeya ako. Piya inasema kama mutu aliye bebwa mahakamani anaweza chongeya ma shahidi (temoins) benyi balisema bitu bibaya ju yake na kuleta bake bashaidi kwa kujiteteya.

Sura ya kumi na ine Sura ya kumi na ine inakataza kufanya ao kutumikisha sheriya zenyi kuvunja haki karibu zote zenyi kuwa ndani ya katiba (Constitution) ya Amerika. Sura ya kumi na ine, alakini, haiamuwe namna gani serkali ndogo zitalinda hizo haki, pamoja na haki yakusambishwa kama ginsi sheriya inaomba. Ni kusema kama sheriya za kulinda hizo haki na haki yakusambishwa kama ginsi sheriya inaomba zinapishana ukiwa mu inchi ndogo fulani ao fulani.
Rights and Responsibilities in the United States

Ready to test your knowledge?

Education Settle in app

Pakua programu ya Settle In

Get unlimited access to hundreds of lessons designed for all learners

Apple Store icon
Get it on Google Play store
Settle In App

Pakua programu ya Settle In

With short videos and interactive lessons, you can learn about a wide range of pre- and post-arrival resettlement topics like traveling to the U.S., housing, and looking for a job.